![](https://globalpublishers.co.tz/wp-content/uploads/2017/06/form-4.jpg)
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Teotimus Swai baada ya mshtakiwa kukiri kosa na hivyo mahakama kumkuta na hatia pasipo shaka.
Kabla ya kusoma hukumu hiyo, mwendesha mashitaka, Baraka Hongoli aliiiambia mahakama kuwa, mshitakiwa alitenda makosa ya kuvunja na kuiba Mei 25 mwaka huu saa mbili usiku nyumbani kwa Veronica Crispin katika Kijiji cha Kalovye, Inyonga.
Aidha, Hongoli aliendelea kusema kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kuvnja nyumba hiyo aliiba nguo zenye thamani ya Sh 110,000 na cheti cha kidato cha nne cha Henreth Edward Kalamu, kilichotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) mwaka 2015.
Mwendesha mashtaka huyo aliiomba mahakama kumpa mtuhumiwa huyo adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine kwani tabia za kuiba vyeti husababisha baadhi ya watu kupoteza kazi zao na hata wengine kufungwa.
Comments
Post a Comment